Ezekiel Kamanga,Chunya.
Wananchi wa kijiji cha Kibaoni wilayani Chunya mkoani Mbeya wanalalamikia viwanda vidogo vidogo vinavyotumika katika kusafishia dhahabu kutoka kwenye mchanga kwa madai kuwa moshi wake umekuwa ukiwasababishia kuwashwa kwenye koo,mafua yasiyo isha na vikohozi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi wa kibaoni wamesema kuwa kwa sasa wanahofia afya zao pamoja mifugo yao kutokana na madhara walioanza kuyapata tangu viwanda hivyo viwekwe karibu makazi yao.
Oswad Mbuya mkazi wa kijiji hicho cha kibaoni alisema moshi huo unaotoka katika viwanda hivyo vya uchenjuaji unawasababishia kupata na mafua ya mara kwa mara,vifua,pua kuwashwa na vikohozi visivyo isha hali inayowalazima kuondoka nyumbani mara tu wanapoanza shughuli hiyo ya kuprosesi dhahabu.
Mkazi mwingine aliyezungumzia sula hili ni Rose Tuli alisema ni kwa muda mfupi tu tukwisha anza kupata madhara na kwamba endapo wataendelea na shughuli hii kwa muda wa miaka kadhaa hatui hatima yetu itakuwaje kwani sasa vifua visivyoisha,mafua vikohozi hata tukinywa dawa hatupati nafuu.
Sabina Thomas alisema wao tu wamekuwa wanaumwa viohozi,mafua,na vichwa hajui mifugo yao wanayoifuga inaathirika vipi kwani wanafuga kuku,ngombe,nguruwe na mbuzi na kwamba wanaomba wataalamu waangalizie huo moshi kama hautakuwa na madhara zai ya hayo maana wanaishi kwa wasiwasi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kijiji cha kibaoni Joshua Mlambalala amekiri kuwepo kwa malalamiko hayo ya wananchi ambapo alisema kuwa wao kama serikali wanasubiri tamko la nemki kwani wamiliki wa viwanda wanaruhusiwa kufanya shughuli hizo baada ya kuruhusiwa na watu wa mazingira kufanya ukaguzi.
Wananchi wa kijiji cha Kibaoni wilayani Chunya mkoani Mbeya wanalalamikia viwanda vidogo vidogo vinavyotumika katika kusafishia dhahabu kutoka kwenye mchanga kwa madai kuwa moshi wake umekuwa ukiwasababishia kuwashwa kwenye koo,mafua yasiyo isha na vikohozi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi wa kibaoni wamesema kuwa kwa sasa wanahofia afya zao pamoja mifugo yao kutokana na madhara walioanza kuyapata tangu viwanda hivyo viwekwe karibu makazi yao.
Oswad Mbuya mkazi wa kijiji hicho cha kibaoni alisema moshi huo unaotoka katika viwanda hivyo vya uchenjuaji unawasababishia kupata na mafua ya mara kwa mara,vifua,pua kuwashwa na vikohozi visivyo isha hali inayowalazima kuondoka nyumbani mara tu wanapoanza shughuli hiyo ya kuprosesi dhahabu.
Mkazi mwingine aliyezungumzia sula hili ni Rose Tuli alisema ni kwa muda mfupi tu tukwisha anza kupata madhara na kwamba endapo wataendelea na shughuli hii kwa muda wa miaka kadhaa hatui hatima yetu itakuwaje kwani sasa vifua visivyoisha,mafua vikohozi hata tukinywa dawa hatupati nafuu.
Sabina Thomas alisema wao tu wamekuwa wanaumwa viohozi,mafua,na vichwa hajui mifugo yao wanayoifuga inaathirika vipi kwani wanafuga kuku,ngombe,nguruwe na mbuzi na kwamba wanaomba wataalamu waangalizie huo moshi kama hautakuwa na madhara zai ya hayo maana wanaishi kwa wasiwasi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kijiji cha kibaoni Joshua Mlambalala amekiri kuwepo kwa malalamiko hayo ya wananchi ambapo alisema kuwa wao kama serikali wanasubiri tamko la nemki kwani wamiliki wa viwanda wanaruhusiwa kufanya shughuli hizo baada ya kuruhusiwa na watu wa mazingira kufanya ukaguzi.
Mlambalala
alisema kuwa watu wa mazingira walishafika katika kijiji chake na
kuchukua michoro kwa wawekezaji wa viwanda na kuwapelekea michoro NEMC
ili kuona jinsi viwanda hivyo vinavyofanya kazi na kuwapa maelekezo.
Kwa
upande wake afisa usafi na mazingira wilaya ya chunya Yohana Ngulukia
alisema kuwa ni kweli viwanda hivyo vipo kwenye maeneo ya makazi ya
watu na kwamba si kitu kinachokubali na kwmba kwa kuondoa malalamiko
hayo wao kama halmshauri wamekwisha tenga hekari 10 katika kata ya Itewe
kwa ajili ya viwanda vidogo vidogo ili kupunguza malalamiko hayo kutoka
kwa wananchi.
Ngulukia amesema wananchi wawe na subira kuhusu kuondolewa kwa viwanda hivyo katika makazi kwani walishawapatia maelekezo wamiliki wa viwanda kutengeneza namna ya kufanya moshi usisambae kwenye maeneo ya watu na kwamba wanamikakati ya kupeleka huduma ya umeme katika eneo lililotengwa kwaajili ya viwanda na maji.
Mwisho.
Ngulukia amesema wananchi wawe na subira kuhusu kuondolewa kwa viwanda hivyo katika makazi kwani walishawapatia maelekezo wamiliki wa viwanda kutengeneza namna ya kufanya moshi usisambae kwenye maeneo ya watu na kwamba wanamikakati ya kupeleka huduma ya umeme katika eneo lililotengwa kwaajili ya viwanda na maji.
Mwisho.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni