Jeshi
la Polisi Zanzibar limewakamata watu wanne wakiwemo vigogo wa Chama cha
Wananchi CUF wakituhumiwa kupanga na kuhusika katika uratibu, utengenezaji na
ulipuaji wa mabomu.
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Naibu Mkurugenzi wa upelelezi na Makosa ya Jinai Zanzibar Kamishina Msaidizi wa polisi Salum Msangi amesema watuhumiwa hao wamekamatwa baada ya upelelezi wa
Watuhumiwa waliokamatwa ni Omar Bakari Nassor,Hassan Omar Issa Mwenyekiti wa CUF wilaya ya Magharibi Salehe Mohamed Saleh Katibu wa CUF Magharibi na Suleiman Mohmaed Bakari Katibu wa CUF Mfenesini.
Mkuu huyo wa upelelezi
amesisitiza na kutoa onyo kuwa Jeshi la Polisi halitasita na linaendelea na
kazi ya kuweka ulinzi kwa wananchi na yeyote au kikundi kitakachojaribu kuleta
fujo polisi imejiandaa kikamilifu.
MALUNDE1/DENICE
Usafi huo umeongozwa na Mkuu wa Wilaya ya
Ilala,Raymond Mushi,Mkurugenzi wa Uuguzi na Ukunga wa Muhimbili, Bi.Agnes
Mtawa pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASCO Mhandisi Cyprian Luhemeja
.
Usafi huo umefanyika katika maeneo yote muhimu ya
Hospitali ikiwemo utoaji wa maji taka .
Akizungumza mara baada ya zoezi hilo, Mkuu wa
wilaya ya Ilala Raymond Mushi amesema zoezi la kufanya usafi halina budi kuwa
endelevu ili kuhakikisha maeneo yote yanakua safi lakini pia kuepuka magonjwa
ya mlipuko ikiwemo kipindupindu.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtawa amewashukuru
DAWASCO kwa uamuzi wao wa kufanya usafi hospitalini hapo ambapo ametumia fursa
hiyo pia kuwaomba wafanyakazi wa Shirika hilo kujitolea kuchangia damu
ili kuokoa maisha ya wagonjwa ambao wanahitaji damu.
FULLSHANGWE/DENICE
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
MOROGORO
Wananchi wa kijiji
cha Dete kata ya Tununguo wilayani Morogoro wamemtaka mkuu wa mkoa wa Morogoro
Dokta Stephene Kebwe kufika kijijini hapo kujionea utendaji kazi wa askari
polisi wa kituo cha Ngerengere.
Ombi hilo limekuja
kufuatia mtu mmoja kuuawa kikatili na watu wasiojulikana bila askari wa kituo
hicho kutoa msaada wowote kwa wananchi.
Wakizungumza wakati
wa kuuondoa mwili wa marehemu Abas Mwarabu aliyekutwa porini akiwa amefariki na
kubaki fuvu na mifupa kutoka na kuchukua muda mrefu tangu alipo uawa wananchi
hao wamesema endapo askari wa kituo hicho hawataondolewa wataandamana hadi kwa
mkuu wa wilaya kupinga utendaji kazi wa askari wa kituo hicho.
ITV/DENICE
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
KIGOMA
Mahakama Kuu Kanda
ya Tabora inayoendelea mjini Kigoma, imemtia hatiani David Kafulila na kumtaka
kulipa gharama kutokana na kukiuka kanuni ya kuwasilisha hati za kiapo
mahakamani, zikiwa zimethibitishwa kama Sheria ya Makosa ya Uchaguzi
inavyoelekeza.

Hata hivyo, kiwango
cha faini anachotakiwa kulipa hakikutajwa ambapo pia kosa hilo halikuzuia
ushahidi wake kupokewa upya mahakamani hapo.
Katika kesi hiyo
aliyoifungua kupinga ushindi wa Hasna Mwilima
wa CCM kuwa Mbunge wa Kigoma Kusini, Kafulila aliyegombea kwa tiketi ya
NCCR Mageuzi analalamika kupokwa ushindi.
Washtakiwa katika
kesi hiyo ni Mwilima ambaye ni mshtakiwa namba moja wakati msimamizi wa
uchaguzi wa jimbo hilo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni washtakiwa namba
mbili na tatu.
Jaji wa Mahakama
Kuu, Ferdinand Wambali amesema Kafulila aliwekewa pingamizi na mawakili wa
utetezi wakimlalamikia kuwasilisha hati ya kiapo iliyokiuka kanuni za
uwasilishwaji kwa mujibu wa sheria.
Jaji Wambali amesema
Kafulila hakutekeleza matakwa ya kisheria ambayo yanaagiza anayewasilisha haki
za viapo kuhakikisha kuwa zimethibitishwa kabla, kwa ajili ya shahidi kuanza
kutoa ushahidi wake.
HABARI24/DENICE
******************************************************************
HABARI ZA KIMATAIFA
GARISSA
Raia
wa Kenya leo wameshiriki kumbukumbu ya kwanza ya shambulizi la kigaidi
lililosababisha vifo vya watu 148, wengi wao wakiwa wanafunzi, katika chuo
kikuu cha Garissa.
Leo
hii kundi la watu 100 wakiwa wamevalia fulana zenye ujumbe wa amani
walikusanyika mjini Garissa, umbali wa kilometa 365, kaskazini mashariki mwa
jiji la Nairobi kwa lengo la kushiriki ibada ya kuwakumbuka wahanga wa mkasa
huo.
Katika
eneo hilo Mbunge wa Garissa Aden Duale amenukuliwa na AFP akisema wapo pamoja
na wazazi, na wanawataka kuwaeleza kwamba kwa pamoja kama taifa lazima
wakabiliane na ugaidi.
Tarehe
kama ya leo mwaka uliopita watu wanne wenye silaha, kutoka kundi la Al-Shabaab
walikizingira chuo hicho, na kuwafyatulia risasi wanafunzi wakiwa katika
mabweni na kuwauwa wengine katika makazi yao.
DWSWAHILI/DENICE
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
WASHINGTON DC
Rais
Barack Obama wa Marekani amesema takribani mataifa 102 yameridhia mkataba wa
ulinzi wa malighafi za nyuklia na ana matarajio ya kuanza kutumika kwake hivi
karibuni.
Aidha
kiongozi huyo ameuonya mkutano wa kilele wa kimataifa kuhusu nyuklia,
unaofanyika nchini mwake kwamba wenye itikadi kali kutoka Kundi la Dola la
Kiislamu "wanawazimu" hawawezi kusita kutumia shambulizi hatari la
kinyuklia.
Kwa
matumani ya kufanikisha hatua za kimataifa kudhibiti makundi ya wenye itikadi
kali kumiliki silaha za nyuklia au malighafi za kile walichoiita "bomu
chafu," Obama alichora taswira yenye kuonesha mfano wa maangamizi ya
ulimwengu kutokana na athari ya shambulizi la nyuklia la kigaidi.
Obama
ambae anamaliza muda wake wa uongiozi mwezi Januari mwakani, amekuwa mwenyeji
wa mkutano wa nne na yumkini ukawa wa mwisho wa viongozi wa mataifa wenye
lengo la kupunguza hatari za kutokea maangamizi ya nyuklia.
DWSWAHILI/DENICE
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
NEWYORK
Azimio hilo lililowasilishwa na Ufaransa limeutaka Umoja wa Mataifa
kuweka mpango madhubuti wa kuwatuma maafisa wa kurejesha amani kwa ushirikiano
na serikali ya Burundi.
Hata hivyo rais wa Burundi , Pierre Nkurunziza, amepinga hatua yoyote ya
kuingilia kati Umoja wa Mataifa na pia Umoja wa Afrika.
Zaidi ya watu 400 wameuawa na robo milioni kutafuta hifadhi katika
mataifa jirani tangu kuzuka kwa vurugu hizo mwaka uliopita.
DWSWAHILI/DENICE
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni