Alhamisi, 2 Juni 2016

KUTOA NI MOYO: MKURUGENZI WA RASI FM RADIO, AMETOA MCHANGO WA MADAWATI 63 KATIKA SHULE YA MSINGI TUBUGWE KIBAONI.....










































Na Peter Mkwavila,Kongwa .
WATANZANIA na Wadau mbalimbali wa elimu wameshauriwa kuchangia kwa kiasi kikubwa kwa hali na mali na nguvu zao,juu ya upatikanaji wa madawati mashuleni ,ili kuwaondolea kero ya wanafunzi  ya kukaa chini badala ya suala hilo kuiachia serikali kufanya  peke yake. 

Ushauri huo umetolewa na mdau wa elimu ambaye pia mkazi wa kijiji cha Tubugwe  Saimon Binde wakati alipokuwa akikabidhi msaada wa madawati 63 kwa mkuu wa wilaya hiyo Bituni Msangi kwa ajili ya shule ya msingi ya Tubugwe Kibaoni iliyopo wilayani Kongwa mkoa wa Dodoma jana.

Alisema kutokana na hadha wanayoipata wanafunzi mashuleni ya kukaa chini juu ya ukosefu wa madawati ,watanzania na wadau wa elimu tunastahili  kuelekeza nguvu zetu katika kuchangia hali na ili kwa ajili ya kuisaidia serikali  ikiwa ni jitihada za kuunga mkono juhudi ya kuliondoa tatizo hilo.

Alisema kuwa hatua ya kuchangia msaada huo wa madawati kwa upande wake ni pamoja na kuwafanya wananfunzi wa shule hiyo ili waweze kufanya vizuri katika taaluma ya elimu ambayo kwa hivi sasa imekuwa ni vigumu kuipata kutokana na walio wengi wamekuwa wakikaa chini.

“Mimi kama mzazi nimeona nisaidiane na serikali ya awamu hii ya tano ambayo imesema inataka kuhakikisha watoto wote kwenye shule zetu hakuna mtoto ambaye atakaye kaa chini kwa ajili ya kukosa madawati,ndiyo maana na mimi nimeamua kuiunga mkono jitihada hizo la kuliondoa kero hiyo ya ukosefu wa madawati mashuleni na  watoto wetu waweze kufanya vizuri kimasomo.”alisema.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya hiyo ya Kongwa Bituni Msangi aliwataka wananchi wa kongwa kuunga jitihada zinazofanywa na serikali ikiwa na pamoja kutumia nguvu zao zitaklazowezesha upatikanaji wa madawati badala suala hili kuachiwa mikononi mwa serikali peke yake.

Alisema juhudi hizo ni pamoja katika kusaidiana uvunaji wa miti inayotengenezwa madawati kuhakikisha wanashirikia kikamilifu kwa kutumia nguvu zao na hata kwa kutoa mali na fedha ili zoezi hilo liendane na kauli ya Rais ambayo amesema mpaka mwezi wa sita hakuna mwanafunzi yoyote ambaye atakayekaa chini kwa kukosa dawati.

Alisema ili kuhakikisha hadhima hiyo inatekelezeka ni muhimu wananchi wa wilaya hiyo wakiwemo na wadau wa elimu wakashirikiana kwa pamoja na serikali,ili kuwaondolea wanafunzi kero hiyo ya kukaa chini ambayo inayowasababishia watoto walio wengi kufanya vibaya masomo yao pamoja na wengine kujikutwa wakipatwa na magonjwa.

“Ninawaomba wadau wengine wajitokeze kama alivyojitokeza mwananchi huyo wa kijiji hiki cha Tubugwe ambaye amejinyima na kutoa fedha zake kwa ajili ya kuisaidia serikali katika kuondokana na kero hii ya watoto wetu ya kukaa chini ambayo imeikubwa karibu shule nyingi hapa nchini”alisema,

Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo ya Tubugwe Kibaoni  Hadija Mohamed alisema kuwa katika shule yake hiyo jumla ya wanafunzi  584 ambao ni wa darasa la kwanza hadi la saba na kwa upande wa watoto wa shule ya awali ni 128 ambapo jumla kuu ni 712.

Alisema wanafunzi wa shule ya msingi ambao kutoka darasa la kwanza hadi la saba wanaokaa kwenye  madawati ni 200 na wanaokaa chini ni 384 na kwa wanafunzi  wa shule ya  awali wote kwa upande wao wanakaa chini,kutokana na idadi hiyo kuwa kubwa ya wanafunzi shule hiyo inahitaji jumla ya madawati zaidi ya 366 ili kuondoa  kero hiyo ya kukaa chini kwa wanafunzi hao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Ad Inside Post