Jumapili, 4 Septemba 2016

WANANCHI WAASWA KUJENGA MAHUSIANO MAZURI NA WAWEKEZAJI

NA: Ezekiel Kamanga,Chunya.

Wananchi na viongozi wa kijiji cha kiwanja kata ya mbugani wilayani Chunya Mkoani Mbeya wameaswa kujenga mahusiano mazuri na wawekezaji wanaofika kijijini kwao ili kuleta maendeleo katika kijiji.

Haya yameelezwa na Afisa  Mazingira Taifa Paul Kalokola wakati akizungumza na viongozi wa kijiji pamoja na wajumbe kijijini hapo mara alipofika  kufanya ukaguzi kwenye eneo la Mwekezaji wa madini ya dhahabu Aidan Msigwa aliyewekeza kijijini hapo.

Ambapo alieleza kuwa kama muwekezaji ameonyesha nia ya kuwekeza ni vyema na wao  wampatie ushirikiano wakutosha kwani kupitia yeye vijana wengi wanaweza kupata ajira na kupunguza ukosefu wa ajira kwa vijana.
 
Kalokola aliendelea kueleza kuwa lengo la wao kufika kwa hapo ni kukagua na kujua mahusiano yaliopo kati muwekezaji huyo na wananchi ili kujirisha pindi wanapo mpatia hati ya  kuendesha kampuni yake.

Akizungumza na mwanachi mjumbe aliyehudhuria kikao hicho  Maneno Ntuma alisema kwasasa hawana mgororo wowote na wanashirikiana nae vyema katika suala zima la maendeleo kwani ameweza kujenga nyumba ya mwalimu yenye uwezo wa kuchukua familia za walimu wawili na kujitoa katika miradi mbalimbali ya kijiji.

Kwa upande wake Mtendaji wa kata hiyo ya mbugani Sadick Kaulule aliwataka maofisa wa mazingira kuwa utaratibu wa kuwatembelea wananchi pamoja na wawekezaji wengine kama walivyofanya ili kuondoa migogoro inayoweza kuepukika kutokana na wananchi kuhofia baadhi ya wawekezaji wanaojishughulisha na uchenjuaji wa madini kwa kutumika kemikali kwania ya kuwatoa hofu miongoni mwao.

Pia aliwashukuru kwa kufika kwao kueleza wao kama vingozi hawana pingamizi lolote kuhusu muwekezaji huyo kuwekeza kijijini kwao kwani amekuwa msaada katika jamii nzima kutokana na kutoa ajira kwa vijana kama wanampatia hati hawezi kuizuia.

MWISHO.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Ad Inside Post